Apr 18, 2016

MWANAMKE AFANYA NGONO NA WANAUME 1,500

MKAZI wa kitongoji cha Chelsea, jijini London,Mare Simone(54) amefanya ngono na wanaume 1,500 katika kipindi cha miaka 23 ili kuwatibu matatizo yanayohusiana na mapenzi.

Wateja ni miongoni mwa wanaume 10,000 waliokwenda ofisini kwake kupata tiba ya matatizo hayo.
Mjasiriamali huyo anatoa ushauri wa mambo ya kimapenzi kwa wanawake na wanaume na ametamba kuwa yeye ni mtaalamu wa masuala ya kitandani.

Baada ya kuachana na mumewe, Mare aliamua kuisomea rasmi taaluma hiyo ya mapenzi na kisha kufungua ofisi na hadi sasa ametoa somo la mapenzi kwa zaidi ya wateja 10,000 waliofika kwenye ofisi yake katika kipindi cha miaka 23.
Mare amebainisha kwamba, kati ya wateja hao,hadi sasa amefanya ngono na wanaume zaidi ya 1,500 wakiwemo waume au wapenzi wa wanawake wengine.

Amesema,hadhani kuwa anafanya kosa lolote kinyume cha sheria kutembea na waume za watu kwa sababu anaboresha maisha ya mapenzi ya watu wengine,anapata riziki yake kwa kutoa tiba hiyo, na kwamba, yeye si kahaba.
"Watu wananilipa kwa ushauri ninaowalipa na kwa kutibu matatizo yao hawanilipi kwasababu ya ngono".
"Najipatia kipato changu kwa kulala na waume au wapenzi wa wanawake wengine.
Lakini mimi sifanyi ukahaba kwa kuwa taaluma ya mapenzi inaruhusiwa kisheria na mapenzi yanafanyika katika mazingira ya tiba" alisema Mare.

"Nasaidia kuimarisha na kubadilisha maisha ya kimapenzi ya maelfu ya wanaume na hivyo nakuwa nimesaidia kuimarisha maisha ya kimapenzi ya wake zao au wapenzi wao"

"Wanawake wengine wanabeba mimba za wanawake wengine kwa sababu wanataka kuwasaidia wanawake wasio na uwezo wa kupata mimba.
Hali hiyo ni sawa na mimi kwani nawasaidia watu kuwa na maisha mazuri ya kimapenzi".

Mare anaifurahia kazi yake na huwa na furaha zaidi wateja wake wanapoondoka kurudi majumbani mwao wakiwa na matumaini mapya kwenye maisha yao ya kimapenzi.

Kwa siku anatoa vipindi vitano vya masuala ya mapenzi,wateja wake ni watu wa rika mbali mbali, jinsia zote, maumbile tofauti na wafanyakazi wa vitengo tofauti tofauti.

"Wanaume mara nyingi hunifuata kwa sababu ya matatizo ya kutosimama vyema kwa uume na kufika kileleni mapema kabla ya wapenzi wao wakati wengine huambiwa waje wanione na wake zao kwakuwa hawawaridhishi kitandani".

"Kabla hawajaniona huwa wote wanapimwa magonjwa ya zinaa na lazima watumie kondomu iwapo nitalala nao" alisema Mare.

"Kwa wanawake mara nyingi hunifuata wakiwa na matatizo ya kutofika kileleni au wanapoona wapenzi wao hawajui jinsi ya kuwaridhisha kitandani".
"Huwa nawafundisha jinsi ya kujipa raha wao wenyewe na kuipenda miili yao" amesema na kusisitiza kwamba hatarajii kuacha kutoa huduma hiyo katika miaka 10 ijayo.

hapo chini ni picha ya mwanamke huyo

BABA AUA WATOTO WATANO

Mwanamume mmoja raia wa Marekani anashukiwa kuwaua watoto wake watano na kuwatupa katika jimbo jingine, hii ni kwa muujibu wa polisi nchini humo.

Timothy Ray Jones anakabiliwa na mashtaka kadhaa katika jimbo ambalo ndio makazi yake la Carolina ya kusini,kufuatia shutuma hizo na alikamatwa mwishoni mwa wiki iliyopita huko Mississippi .

Watoto hao watano waliopoteza uhai kwa kuuawa na baba yao walikua na umri wa kuanzia mwaka mmoja hadi miaka nane inaelezwa watoto hao watano walipotea katika mazingira ya kutatanisha , mama wa watoto hao aliporipoti polisi baada ya mawasiliano kati yake na mzazi mwenziwe kukatika.

Maafisa hao wa polisi walipofanya uchunguzi wao waligundua miili ya watoto hao imezikwa karibu na mji wa Alabama karibu na barabara kuu baada ya kuwasaka watoto hao kwa siku nzima .

Jones alisimamishwa katika kizuizi cha barabarani na kushukiwa kua alikua akiendesha gari baada ya kutumia dawa za kulevya ,imethibitika kuwa katika gari yake kulikuwa na kemikali zinazoaminika kua dawa za kulevya, zaidi ya hapo polisi walikuta damu garini mwake na alikua akitafutwa huko Carolina ya kusini .

Kitengo kinachoshulikia usalama wa raia huko Alabama kimesema kupitia kwa msemaji wake sajenti Steve Jarrett kwamba baada ya msako huo Jones baba wa watoto hao aliwaongoza maafisa hao hadi eneo alikozika miili ya wanawe(picha hapo chini ni ya mtuhumiwa huyo)

mshirikishe na mwenzio

BIBI AZAA NA MJUKUU WAKE


    Bibi mwenye umri wa miaka 72 wa nchini Marekani amewashangaza marafiki zake na familia yake baada ya kutoboa siri kuwa anatarajia kuzaa mtoto na mjukuu wake mwenye umri wa miaka 26.
Bibi Pearl Carter, 72, anasema kuwa hajawahi kuwa mwenye furaha kama wakati ambao amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mjukuu wake Phil Bailey mwenye umri wa miaka 26.

Bibi huyo wa Indiana, Marekani anatumia pesa zake za pensheni kumlipa mwanamke atakayejitolea kuibeba mimba yake na mjukuu wake.

Bibi Pearl alisema kuwa hajali maneno ya watu kuhusiana na uhusiano wake wa kimapenzi na mjukuu wake na anasubiria kwa hamu kuzaa naye mtoto.

Phil ni mjukuu wa bibi Pearl kwa mtoto wake wa kike Lynette Bailey ambaye alipelekwa kwenye nyumba ya kulea yatima alipokuwa na umri wa miaka 18.

Wakati mama yake alipofariki, Phil alimtafuta bibi yake ambaye alikuwa hana mawasiliano naye kwa muda mrefu na ghafla walianza uhusiano wa kimapenzi.

"Ilikuwa ni wiki ya pili pamoja baada ya chakula na mvinyo nilipomuita Phil chumbani kwangu, nilimkalisha kitandani na kuanza kumbusu", alisema bibi Pearl.

"Nilitarajia angenikatalia lakini naye alianza kunibusu" Pearl alisema akielezea mwanzo wa uhusiano wa kimapenzi na mjukuu wake.

"Kwa mara ya kwanza nilijihisi kwenye msisimuko mkubwa wa kimapenzi", alisema bibi Pearl.

Phil naye kwa upande wake anasema kuwa anampenda sana bibi yake na kwakuwa tangia zamani alikuwa akiwapenda wanawake wazee anadhani bibi yake ni mrembo sana.

Phil na bibi yake wametumia dola 54,000 kumlipa mwanamke atakayebeba ujauzito wao.

"Ni kweli tunachekwa na kutukwana wakati tunapobusiana mbele za watu lakini hatujali kitu", alisema Phil.

"Sitamuomba radhi mtu yoyote kwani naamini Mungu amenipa nafasi ya pili", alimalizia kusema bibi Pearl.