May 11, 2016

MADHARA YA KUPENDA USIPOPENDWA

Mapenzi si kamari, ridhia kwa moyo! Ni sentesi ambayo kama mtu akitafakari kwa kina kuna kitu kitaingia kichwani kwake, kuna baadhi ya watu huwa wanabahatisha katika mapenzi, unakuta mtu anakuwa na mpenzi bila kujua kama anapendwa kweli.

Mapenzi ni ridhaa, yanatokea moyoni,

Unajua moyo wako ndiyo wenye uwezo wa kufanya uchaguzi sahihi na si uchaguzi bali uamuzi wa moja kwa moja, maana moyo ndiyo wenye uwezo wa kupenda na kuhifadhi pendo ndani yake, kabla hujaanzisha uhusiano jaribu kuzingatia yafuatayo kwani Mapenzi ya kulazimisha yana madhara kama ambavyo Mtembezi Mahaba inakudadavulia.

MOYO WAKO UMEMPENDA? Suala la mapenzi uhusisha moyo zaidi, moyo wako ndiyo mwamuzi wa mwisho katika hilo, hata siku moja usikubali kulazimisha moyo wako kwa mtu ambaye hujaridhia kuwa naye, hivyo achana na imani kwamba ukimkataa kijana fulani basi bahati inaweza kukupita; nani amekudanganya?

SI KAMARI

Utakuta msichana anaingia katika uhusiano na mwanaume ambaye hana mapenzi naye ya dhati lakini kwa kuwa mwanaume huyo ana mali na uwezo wa fedha, huamua kumkubali kwa misingi ya kuwa na tamaa ya mali zake, hufanya hivyo akijidanganya kuwa atajifunza kupenda akiwa ndani ya uhusiano na mwanaume huyo kwa maneno mengine, anajidanganya kwamba atacheza kamari ya mapenzi.

MADHARA YA KAMARI YA MAPENZI!

Yapo mengi, lakini kubwa ni lile la kutotosheka na mpenzi uliyenaye; anaweza akakupa kila kitu lakini ukakosa penzi la dhati, ambalo ndiyo msingi wa mapenzi.

Mapenzi ya kweli siku zote utajisikia mwepesi na huru kwa mwenzako, madhara makubwa zaidi ni pale utakapojikuta ukiingia katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa ajili ya kusaka penzi la dhati! Unajua kitakachotokea?

Kama hutaleta magonjwa ndani basi siku moja utafumaniwa, kuna siku lazima utafukuzwa nyumbani kwa mwanaume huyo na kama ana hasira, anaweza kukufanyia kitu kibaya, hivyo ni vyema kufanya uamuzi wa busara kwa kuwa na mahusiano na yule akupendaye.

KASI YA MAGUFULI YAWAANDIKISHA BARUA ZA KUJIUZURU WATUMISHI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na

Simbachawene amesema kasi ya Rais Dkt John

tayari watumishi wameanza kuandika barua za kuomba kujiuzulu na kutafuta kazi sehemu nyingine.

Waziri Simbachawene ameyasema hayo ingawa hajataja majina ya watumishi hao na halmashauri wanazotoka, katika kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na ITV na

ameshapokea

kutoka

watatu

ambao hawana

kiutendaji

barua ya kuomba kuachia kazi hizo.

”Kasi ya Rais Dkt. Magufuli haitawaacha watumishi

kufanya kazi kwa maana mazoea kazini hayapo

nimeshapokea

watatu wakiomba kujiuzulu nyazifa zao na kweli kama kuna kiongozi anaona hataweza kwenda na kasi ya Rais na Wizara yangu ni bora aondoke mapema kabla

nitawatumbua

Chawene.

MSANII KINYAMBE AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji aliyekuwa anakuja juu kwa kasi Mohammed Abdallah  "KINYAMBE" amefariki dunia leo usiku huko nyumbani kwako Mbeya.

Mmoja wa wanandugu wa Kinyambe ameithibitishia saluti5 kuwa msanii huyo wa filamu  ambaye pia alikuwa akijulikana kwa jina la James, amefariki baada ya kuugua kwa siku kadhaa.

"BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA MUNGU LIHIMIDIWE".

MUIMBAJI SHILOLE ATAJA MPENZI WAKE WA SASA

Uking’atwa na nyoka ukiguswa na jani lazima utaruka.Baada ya kuvunjika kwa mahusiano na Nuh Mziwanda, taarifa za chini zimezidi kuenea kuwa Shilole ana mahusiano ya kimapenzi na msanii chipukizi wa Bongo Fleva, Nerd aliye chini ya label ya Ommy Dimpoz, PKP.Akiongea kwenye kipindi cha Busati, kinachoruka kupitia Magic FM, Shilole amesema hana mpenzi kwa sasa.“Mimi mpenzi wangu ni hela, Nerd ni rafiki yangu. Ukiwa kwenye mapenzi unakuwa kama kipofu unakuwa hauoni. Ukimkabidhi mtu moyo wako anakuwa anaufinyanga, kwa sasa moyo wangu umestawi tofauti na zamani,” aliongeza.Hata hivyo Shilole amesema hana namba ya Nuh Mziwanda na hajawahi kuwasiliana naye tangu walipoachana. Kwa sasa muimbaji huyo ana wimbo mpya uitwao Say MyName.

BINTI WA MIAKA 19 ANAEDAI KUA NA MIMBA YA PAPA WEMBA AJITOKEZA HADHARANI

Binti wa miaka 19 anadaiwa kuspend one night on the same bed na Hayati Papa Wemba amekua gumzo kwenyemitandao ya kijamii ndani na nje ya Congo(D.R.C) akidai kuwa na ujauzitowa Mfalme huyo wa Rhumba aliefarikiApril 24 mwaka huu baada ya kuanguka jukwaani jijini Abidjan nchini Ivory Coast.Picha zinazodaiwa kuwa copied kutoka kwenye akaunti za social media za binti huyo,zinamuonesha akiwa kwenye pozi tofauti za kimahaba na Papa Wemba,picha ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya picha hizo zikionesha tumbo lake na nyingine zikimuonesha akikiss na Hayati Papa Wemba.Mpaka sasa hakuna taarifa yeyote rasmi kutoka kwenye familia ya Papa Wemba juu ya madai ya binti huyo ambae baadhi ya mashabiki wa Mfalme huyo wa Rhumba wameahidi kumsaidia kwa lolote hadi atakapojifungua.

HARMONIZE:MIMI NA DIOMOND TUNATOFAUTI

Kwenye miaka ya 2000 staili ya kuchana ilishika hatamu ambapo msanii kama TID, Mangwea, Profesa J, Juma Nature, Fid Q, Afande Sele na wengine kibao walitikisa game ya muziki wa Bongo Fleva huku kila mmoja akiwa na staili yake inayomtambulisha na kufanya wajulikane na kupata umaarufu.

Hivi sasa game ya Bongo Fleva dizaini kama ladha unapotea siku hadi siku kutokana na kuwepo kwa baadhi ya wasanii kuigana sauti kama ambavyo imekuwa ikidaiwa na baadhi ya mashabiki wa muziki huo, Hit Maker wa wimbo wa Aiyola kuwa moja kati ya wasanii wanaomuiga sauti Star wa Bongo ambaye pia ni meneja wake DIAMOND PLATNUMZ kupitia 255 ya XXL Harmonize amesema

“Ukizungumzia Diamond unazungumzia mtu ambae anamelody ya malalamiko ambayo zimeganda kwenye vichwa vya watu wengi kwa hiyo ukiimba malalamiko lazima utafananishwa, lakini huu ni wakati mzuri wa kutambua huyu ni Harmonise huyu ni Diamond”

Baada ya kufanya kolabo ya ngoma ya Bado iliyobamba na kumuweka Harmonize katika nafasi nzuri kimuziki hivi karibuni amezawadiwa gari aina ya Mark X kutoka kwa uongozi wa WCB.

JE UNAJUA KAMA KUFLASH SIMU NIKOSA LA JINAI?

Kumekuwa na tabia kwa baadhi ya watu ‘kuflash’ simu kunakosababishwa na sababu kadha wa kadha; katika zama hizi za utandawazi vitendo vya watu kuporwa simu za mkononi vimeripotiwa kwa kiasi kikubwa na wengi wao waliona kuwa njia sahihi nikuziflash ili zitumiwe na mtu mwingine bila kujua kuwa ni kosa la jinai kutokana na sheria za mtandao.

Hayo yamebainika wakati zimesalia siku 36 pekee ili Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) kuzima simu zote ambazo hazijakidhi viwango huku Meneja Mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy akisisitiza watu kuacha mara moja tabia hiyo kwani kwa kufanya hivyo kutapelekea simu zao kuzimwa ifikapo June mwaka huu kwa kuwa tayari zitakuwa zimetolewa ubora wake.

“Unapoflash simu lazima fundi atakubadilishia Software zilizokuwepo toka mwanzo alafu utakuwa umeharibu ubora wa kile alichotengeneza mwanzo hivyo kutokana na sheria za umiliki unakuwa umetenda kosa la jinai”. Alisema Mungy

Mamlaka ya Mawasiliano imetoa rai kwa wanaonunua simu za mkononi kwa wakati huu wa lala salama kuwa makini kwa kuangalia namba za IMEI kwa kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanapunguza bei za simu feki.

BAADA YA MIAKA 46 YA NDOA MWANAMKE MWENYE UMRI WA MIAKA 70 AJIFUNGUA

Baada ya miaka 46 ya ndoa, mwanamke mwenye miaka 70 amejifungua mtoto wa kwanza huko India..Daljinder Kaur amejifungua mtoto wa kiume baada ya kupata matibabu ya IVF kwenye kliniki za uzazi huko India.Kwenye picha akiwa na mume wake wa miaka 79, Kaur alisema yeye na mume wake walikuwa karibu kukata tamaa ya kupata mtoto kutokana na umri wao na kuona Kama Mungu amewalaani wasipate mtoto.Alisema hatimae Mungu amejibu maombi yao na wamepata mtoto na sasa wanajiona wamekamilika.Aliendelea kusema kuwa yeye na mume wake watamlea mtoto wao wenyewe kwasababu huyo mtoto amewapa nguvu mpya katika maisha.Pia anawasihii wote wenye changamoto za uzazi wamuombe Mungu bila kuchoka.... Aliongezea kusema....".....I can't wait to b a grandma!!

TP MZEMBE WAMLILIA SAMATTA

Jina la Mbwana Samatta limeacha historia kubwa nchini DR Congo hususani kwa mashabiki wa Klabu ya TP-Mazembe ambao wameshuhudia timu yao ikishindwa kufanya vizuri kwenye michuano ya Klabu Bingwa. Hapa ndio inaeleweka ni kwa nini Rais wa Timu hiyo Moise Katumbi alikuwa hataki kumwachia Mbwana Samatta.

Mazembe ilitolewa na Wydad Casablanca ya Morocco katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa na kuangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Thomas Ulimwengu amesema kwamba kwa sasa pengo la Mtanzania mwenzake, Mbwana Ally Samatta linaonekana ndani ya TP Mazembe. Ulimwengu alisema TP Mazembe kwa sasa inamkosa mtu mjanja na mwepesi, mwenye uwezo wa kufunga kama Samatta.

Samatta aliondoka timu hiyo ya DRC Januari mwaka huu baada ya kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Afrika na kujiunga na KRC Genk ya Ubelgiji anakoendelea vizuri hivi sasa.

MAKONDA AFICHUA SUKARI ILIYO FICHWA GOROFANI

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda wamegundua Sukari iliyofichwa katika jengo la ghorofa tisa ambalo liko katika jengo linalojengwa katika eneo la Hananasifu -Kinondoni huku mmiliki wa sukari hiyo Bw,Bashir Ismail mwenye asili ya kiasia akitiwa mbaroni na jeshi la Polisi.

Sukari hilo inadaiwa kuingizwa usiku katika jengo hilo huku kikiwa katika mifuko ya viroba vya kilo 25,na ishiri lakini pia ikifungwa katika mifuko midogo ya Plastiki ya kilo moja moja.

Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari amesema baadhi ya wafanyabiashara wameendelea kukaidi agizo la serikali kwa kuficha sukari katika maghara na maeneo mbali mbali na kuahidi kuwa Oparesheni dhidi ya wafanyabiashara hao ni ya kudumu.

Bw, Bashir Ismail ambaye alikuwa chini ya Ulinzi wa jeshi la Polisi alihojiwa na kudai sukari hiyo iliyohifadhiwa katika jengo hilo inapelekwa katika vituo vya kijamii ingawa alishindwa kujieleza jinsi mazingira iliyowekwa huku ikifanyika kazi ya kuweka katika viroba kwa kuwa eneo hilo linafanyika ujenzi na sio kiwandani.