LICHA ya tetesi kuzagaa kuwa amerudiana na
mpenzi wake, Idris Sultan, mtoto mzuri Bongo
Muvi, Wema Sepetu kwa mara nyingine
ametengeneza habari, amedaiwa bado
anaendeleza uhusiano wa siri na staa wa
Bongo Fleva, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’,
Hiyo imedhihirika hivi karibuni baada ya
kuvuja kwa picha mpya za wawili hao wakiwa
chumbani katika mapozi ya kimahaba huku
1)Picha moja wapo ilimuonesha Dimpoz akiwa
amemwekea miguu Wema mgongoni huku
nyingine akiwa ameegesha mkono kwenye
kalio kitendo ambacho kinaleta tafsiri ya mtu
na mtu wake.
Dimpoz amekuwa akiendelea ‘kujiweka’ kwa
siri jambo ambalo watu wengi hawalitambui.
“Mbona kitambo tu, Dimpoz amejiweka kwake
kiulaini, sema wenyewe wanafanya mambo
hayo kwa siri. Si mnajua Dimpoz si mtu wa
kutangazatangaza mambo yake na ndiyo
maana hadi Nay wa Mitego (Emmanuel Elibariki) akafikia hatua ya kumhisi vibaya
hadi kumuimba kwenye wimbo wake,”
kilisema chanzo
MAZINGIRA YA TUKIO
Chanzo hicho kilimwaga ubuyu kuwa, picha
hizo walipiga wenyewe chumbani, nyumbani
kwa Dimpoz, Kinondoni jijini Dar hivyo zilibaki
katika simu ya Dimpoz ndipo chanzo hicho
kilipozikwapua na kuzituma kwa paparazi
wetu.
“Bwana nakupa lakini msinitaje huko, nyie
kamilisheni mambo yenu lakini habari ndiyo
hiyo; Dimpoz na Wema ni kapo ya kimyakimya
maana wenyewe hawataki kuanika mambo
yao,” kilisema chanzo hicho.
WEMA ASAKWA
Baada ya kupata ubuyu huo, Reporter wetu
‘alimvutia waya’ Wema ili kumsikia
anazungumziaje picha hizo na uhusiano huo
unaodaiwa ni wa siri, simu yake iliita bila
kupokelewa lakini baadaye rafiki yake mmoja
alisema huenda hakupokea kwa kuwa siku
hiyo alikuwa safarini kuelekea Dodoma.
“Jana (Jumatano) aliniaga ana safari ya
Dodoma so (hivyo) nafikiri yupo njiani na
wenzake na pengine kelele za wasanii ndani
ya gari si unajua tena na kaenda na wasanii
wenzake wengi tu,” alisema rafiki huyo
ambaye hakupenda jina lake lichorwe
gazetini.
DIMPOZ HUYU HAPA
Baada ya kumkosa Wema, Repoter wetu
alimtafuta Dimpoz ambaye alikiri kuwa picha
hizo zilikwapuliwa kutoka kwenye simu yake
lakini akadai hawana uhusiano wa kimapenzi.
“Hizo picha nazijua, nakumbuka tulipiga
hapahapa Dar. Ilikuwa ni hotelini na si
nyumbani kama huyo mtu alivyowaambia
lakini kitu cha msingi unachopaswa kujua,
Wema ni mshikaji wangu wa karibu na hakuna
kitu kingine zaidi ya ushikaji. Kuna mtu
itakuwa kanifanyia umafia kwenye simu lakini
nitadili naye lazima nitamjua tu,” alisema
Dimpoz.
KUMBUKUMBU
Wema na Dimpoz walidaiwa kuanzisha
uhusiano wa kimapenzi, Februari, mwaka jana
walipokuwa wakirekodi video ya Ommy,
Wanjera nchini Afrika Kusini.
Picha zao ‘tata’ wakiwa chumbani zilizagaa
kwenye mitandao ya kijamii na kuripotiwa
katika vyombo vya habari.
Baada ya hapo, Wema aliripotiwa kutembea
na wanaume tofauti akiwemo Idris Sultan,
mshindi wa Shindano la Big Brother Africa.
No comments:
Post a Comment